Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na nchi. Aliumba jua, mwezi, na nyota, na pia mimea na wanyama. Siku ya sita, aliumba mtu kwa mfano wake na akampulizia puani pumzi ya uhai. Mtu huyu wa kwanza alikuwa Adamu, na jina la mkewe aliitwa Eva. Mungu aliwapa makao ya kuishi katika bustani nzuri ya Edeni. Mungu aliwapenda Adamu na Eva, nao walimpenda Mungu. Mungu alimwagiza Adamu kuitunza bustani. Mungu aliwaambia kua wanaweza kula chochote watakacho isipokuwa kwa mti wa ujuzi wa mema na mabaya, na ya kuwa watakufa kama hawatatii.
22 Septemba 2025 in Baadaye, Injili, Mbinguni, Color 3 minutes
Imeandikwa na John Reynolds Mojawapo ya mifano iliyohai na ya kuvutia kabisa ya kurudishiwa uhai wa mtu aliyekwisha kufa ambao nimewahi kuufahamu ulikuwa ni ule wa George Lennox, mwizi stadi wa farasi kutoka Jimbo la Jefferson (Marekani). Alikuwa akitumikia kifungo chake cha pili. Jimbo la Sedwick lilimpeleka gerezani kwa mara ya kwanza kwa kosa hilo hilo – wizi wa farasi.
22 Machi 2019 in Baadaye 11 minutes