Maisha Ya Kikristo
Je, wajua kwamba kuna kitabu ambacho hueleza jinsi dunia ilivyoanzishwa? Maneno ya kwanza ya kitabu hiki ndiyo, “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi”. Kufuata maneno haya inaeleza jinsi dunia ilivyoumbwa na kuhusu mwanamume wa kwanza na mwanamke walioishi duniani. Inatuambia si tu kuhusu mwanzo wa muda, lakini pia ni kile kitakachotokea maisha haya yakiisha. Katika kitabu hiki chote, twasoma jinsi tunavyopaswa kuishi ili tuandaliwe kwa maisha baada ya kifo.
Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembaba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo. Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache. Mathayo 7:13-14 Umeshikilia ramani ya maisha. Maisha yetu ni safari. Hapa duniani tunapitia tu. Mungu anapoifikisha safari yako mwisho wake, ni hatima gani inakusubiria katika umilele? Unaona katika maandiko kwamba kuna njia mbili tu. Njia hizi mbili zaelekea katika hatima mbili tofauti. Mungu anakupenda na anakuwazia mema. Anataka uwe naye mbinguni, lakini anakuachia kufanya uchaguzi. Sasa, hebu tuchunguze ramani hii ili tufanye uamuzi sahihi.
Tunaishi katika ulimwengu ambamo kila mmoja hupenda kutoa udhuru. Karibu kwa kila jambo linalogusa moyo wako hutaki kukubali au kuukabili ukweli jinsi ulivyo, kwa hiyo unatafuta njia ya kujitetea, ukidhania kwamba utetezi wako utakuweka huru. Je, unafikiri udhuru zako zitakuweka huru mbele za Mungu? Je, kuokolewa kunao udhuru? Visingizio ulivyo navyo kwa uhakika havitakuweka huru. Adamu na Hawa walipotenda dhambi, kila mmoja alijaribu kumtupia mwenzake lawama ya dhambi iliyotendeka, wakidhania kwamba Mungu angeachilia dhambi yao kwani wametoa sababu ni kwa nini waliingia dhambini. Lakini bado twasoma katika Biblia kwamba Mungu aliendelea kuwaadhibu tu. Mungu hazikubali udhuru zetu, hata zipangiwe kwa hila ya namna gani, au hata ukijifanya uonekane kuwa msafi kiasi gani. (Mwanzo 3:9-19; Wagalatia 6:7-8).
Kila mahali watu wote hutamani kuwa na vitu vya kupendeza kwa maisha yao. Kila mmoja angependa kuwa na chakula kizuri, na cha kutosha kugawanya kwa marafiki na wageni; nguo zilizokamilika, na za kutosha kubadili kwa wakati mbalimbali; nyumba nzuri, imara na kubwa ya kutosha, yenye paa nzuri kwa majira yote. Pia tunatarajia kuwa na kiasi cha fedha mkononi ili kukabili matumizi yote, shughuli zetu, kwa dawa ukijitokeza ugonjwa, na hata ya kutosha kusafiria kuwaona marafiki mahali pengine. Kila mmoja hutaka dhamana ya kufanikiwa, hata kuwa na pesa za ziada mkononi kumaliza shida za dhorura.