Africa

Mwanamume mmoja kijana alifiwa mke wake wakati mtoto wake wa kiume akiwa bado mdogo. Kwa maangalizi ya makini na ya woga kabisa huyo baba aliweza kumlea yule mtoto. Kwa kuwa kijana alikuwa ni mboni ya jicho lake, alimpa vitu vingi, na alimpa chakula bora kabisa kilichokuwa kinapatikana. Baada tu ya yule mwanaume kupona na mawazo ya kumpoteza mke wake mpendwa, mtoto wake wa kiume aliugua na alikuwa na hali mbaya sana. Daktari aliagiza dawa ya kuponya ugonjwa wake. Dawa ile ilikuwa na ladha ya uchungu, kwa hiyo yule kijana hakutaka kuinywa. Kila mara baba yake alikuwa anamlazimisha kunywa ile dawa.

23 Septemba 2025 in  Yesu, Africa 2 minutes

Hili ni swali zuri sana ambalo kila mmoja anapaswa kujiuliza. Biblia inaongelea njia kuu mbili tu; njia ya kwenda Mbinguni na njia ya kwenda Jehanamu. Mbinguni ni sehemu yenye kila kitu kizuri, na ni makao ya Mungu. Jehanamu ni mahali pa dhambi na maharibifu yasiyo na mwisho. Ni sehemu iliyoandaliwa kwa ajili ya Shetani na watoto wake. Je,nifanye nini ili niweze kufika mahali ambapo ni nyumbani mwa Mungu? Kama wewe si mkristo sahihi, na haujazaliwa kwa mara ya pili, basi unahitaji wokovu.

16 Septemba 2025 in  Wokovu, Africa 6 minutes

Mungu wa Kweli Ndiye Muumbaji

Tunasoma katika Biblia, “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Na Mungu akawabarikia” (Mwanzo 1:27-28). Mungu alimwumba mwanadamu, uumbaji wake wa hali ya juu kabisa na wa hekima, “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai” (Mwanzo 2:7). Anastahili wanadamu wamtumikie na kumsifu Yeye. “Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa” (Ufunuo 4:11). Kwa hiyo, viumbe vyake vingemwabudu Yeye, na Yeye tu, “…kumwabudu katika roho na kweli” (Yohana 4:24).

Hindi Rundi

23 Mei 2024 in  Yesu, Africa 6 minutes

Je, ni kwa “njia ya Yesu Kristo”? Au ni kwa “njia ya kimwili”? Njia ya Yesu Kristo ni njia nyembamba. Inaongoza kwenda Mbinguni. Huko Mbinguni hakutakuwa na huzuni wala maumivu, bali furaha na faraja pamoja na Yesu na malaika watakatifu. Njia ya kimwili ni njia pana. Inatuelekeza kwenye maangamizi, yaani Jehanamu, mahali ambapo kutakuwa na maumivu, maombolezo, na kusaga meno. Ili kuenenda katika njia ya Yesu Kristo, lazima tuachane na njia ya kimwili. Yesu alisema, “Mtu yeyote akitaka kuwa mfuasi wangu, lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.” (Mathayo 16:24). Je, kujikana nafsi kunamaanisha nini?

23 Mei 2024 in  Baadaye, Africa 4 minutes

Kila mahali watu wote hutamani kuwa na vitu vya kupendeza kwa maisha yao. Kila mmoja angependa kuwa na chakula kizuri, na cha kutosha kugawanya kwa marafiki na wageni; nguo zilizokamilika, na za kutosha kubadili kwa wakati mbalimbali; nyumba nzuri, imara na kubwa ya kutosha, yenye paa nzuri kwa majira yote. Pia tunatarajia kuwa na kiasi cha fedha mkononi ili kukabili matumizi yote, shughuli zetu, kwa dawa ukijitokeza ugonjwa, na hata ya kutosha kusafiria kuwaona marafiki mahali pengine. Kila mmoja hutaka dhamana ya kufanikiwa, hata kuwa na pesa za ziada mkononi kumaliza shida za dhorura.

Kinyarwanda Rundi

23 Mei 2024 in  Maisha Ya Kikristo, Africa 10 minutes