Amani
Amani, amani iko wapi—kwa mataifa, nyumbani kwetu, na zaidi ya yote kwa mioyo yetu? Kilio hiki kikuu kimesikika kwa vizazi. Je, ni kilio cha moyo wako pia? Watu wamechoka na kuhangaika. Bila shaka kuna haja ya mwongozo na ushauri, usalama na kujiamini. Tunahitaji na kutaka akili yenye utulivu. Akili yenye utulivu—Ni hazina iliyoje! Je, hazina hii inaweza kupatikana katika ulimwengu wenye mizozo na kukata tamaa, wenye misukosuko na matata?
Hofu ni nini? Hofu ya Mungu Hofu ya wakati ujao Hofu ya kushindwa Hofu ya mateso Hofu ya kifo Hofu, adui wa siri, huvamia watu wa kila umri na utaifa, na kila hatua ya maisha. Ni hila na ya kuumiza, hutia sumu namna yetu ya kufikiri, huiba furaha yetu ya ndani, na huua hamu yetu ya kuishi. Inatufanya tuwe na wasiwasi, wanyonge, wenye mshituko, wenye mahangaiko, kukasirika na wenye moyo dhaifu: Ni hisia gani hizi mbaya sizizohitajika!
Maisha ni magumu. Mateso na magumu ni sehemu ya maisha yetu. Watu wengi kwa wakati mwingine wanaugulia magonjwa ya kimwili. Njaa inawashikia watu kwa asilimia kubwa hapa duniani. Umasikini unawatesa watu wasio na uwezo. Na wengine wapo wanaoteseka mikononi mwa watu kwa namna mbalimbali. Kwa mfano, baadhi wanashikwa na matatizo ya kindoa, au wazazi wakatili, au mabwana wakali. Kwa sababu ya hali ya vita katika baadhi ya nchi zingine watu wengi wasio na hatia wanapoteza mali, nyumba, familia, na hata maisha yao. Wale wanaomtumikia Mungu kwa uaminifu, wanateswa na kuudhiwa kwa sababu ya imani yao. Ulimwenguni pote watu mamilioni wanateseka kila siku. Kwa nini?