Yesu
Mwanamume mmoja kijana alifiwa mke wake wakati mtoto wake wa kiume akiwa bado mdogo. Kwa maangalizi ya makini na ya woga kabisa huyo baba aliweza kumlea yule mtoto. Kwa kuwa kijana alikuwa ni mboni ya jicho lake, alimpa vitu vingi, na alimpa chakula bora kabisa kilichokuwa kinapatikana. Baada tu ya yule mwanaume kupona na mawazo ya kumpoteza mke wake mpendwa, mtoto wake wa kiume aliugua na alikuwa na hali mbaya sana. Daktari aliagiza dawa ya kuponya ugonjwa wake. Dawa ile ilikuwa na ladha ya uchungu, kwa hiyo yule kijana hakutaka kuinywa. Kila mara baba yake alikuwa anamlazimisha kunywa ile dawa.
Mungu wa Kweli Ndiye Muumbaji
Tunasoma katika Biblia, “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Na Mungu akawabarikia” (Mwanzo 1:27-28). Mungu alimwumba mwanadamu, uumbaji wake wa hali ya juu kabisa na wa hekima, “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai” (Mwanzo 2:7). Anastahili wanadamu wamtumikie na kumsifu Yeye. “Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa” (Ufunuo 4:11). Kwa hiyo, viumbe vyake vingemwabudu Yeye, na Yeye tu, “…kumwabudu katika roho na kweli” (Yohana 4:24).
Je, wajua kwamba kuna mtu ambaye hujua yote juu yako? Ni Mungu aliyeumba ulimwengu na vitu vyote vilivyomo. Yesu, Mwana wa Mungu, pia hujua yote ambayo umeshafanya. Yeye hujua yaliyopita, ya leo, na yajayo. Yeye anakupenda na alikuja ulimwenguni kukuokoa kutoka dhambini. Anao mpango wa uzima wako ili kukuletea furaha. Siku moja Yesu alikuwa akitembea na rafiki zake alifikia kijiji cha Samaria. Yesu alikaa kando ya kisima wakati rafiki zake walienda kununua chakula. Yesu alipokuwa amekaa pale, mwanamke mmoja alikuja kuteka maji kisimani. Yesu alimwambia, “Naomba unipe maji ninywe.”
Je, wewe ni mwenye furaha? Au hofu na hatia huondoa furaha yako yote? Je, ungetamani kuondoa hatia yako, lakini hujui kwa njia gani? Huenda unajiuliza, “Je, nitawahi kuwa mwenye furaha tena?” Ninayo habari njema kwa ajili yako. Kuna Mmoja awezaye kukusaidia, kusamehe dhambi zako, na kukupa furaha ya daima. Jina lake ni Yesu. Ngoja nikuambie habari zake. Mungu ndiye mwenyewe aliyeumba ulimwengu na vitu vyote vilivyomo. Alikuumba wewe na mimi.
Yesu Rafiki Yako Ninaye rafiki. Yeye ndiye rafiki bora ambaye nimewahi kujua. Yeye ni mwema sana na mkweli ambaye na wewe pia ningependa umfahamu. Jina lake ni Yesu. Cha kustajaabisha ni kwamba na yeye angependa awe rafiki yako. Ngoja nikuambie habari zake. Tunasoma hadithi hii katika Biblia. Biblia ni kweli. Ni neno la Mungu. Mungu ndiye aliyeumba ulimwengu na vitu vyote vilivyomo. Yeye ni Bwana wa Mbinguni na dunia. Anatoa uzima na pumzi kwa viumbe vyote.
Kabla ya muda haujakuwepo Mungu alikuwepo. Aliumba dunia na kila kitu kilichomo. Katika upendo wake, Mungu akaumba mwanadamu kwa sura yake mwenyewe akawaweka kwenye bustani nzuri. Wanadamu hawakutii maelekezo ya Mungu. Kutokutii huku kulikuwa ni dhambi iliyowatenganisha mbali na Mungu. Aliwaambia kwamba wanapaswa kutoa dhabihu za wanyama wadogo wasio na madoa yoyote kwa ajili ya dhambi zao. Dhabihu hizi hazikulipia dhambi zao bali zilielekeza dhabihu ya mwisho ambayo Mungu angetoa. Siku moja Mungu angetuma mwanawe Yesu duniani awe dhabihu ya mwisho.