Vipeperushi

Je, ni kwa “njia ya Yesu Kristo”? Au ni kwa “njia ya kimwili”? Njia ya Yesu Kristo ni njia nyembamba. Inaongoza kwenda Mbinguni. Huko Mbinguni hakutakuwa na huzuni wala maumivu, bali furaha na faraja pamoja na Yesu na malaika watakatifu. Njia ya kimwili ni njia pana. Inatuelekeza kwenye maangamizi, yaani Jehanamu, mahali ambapo kutakuwa na maumivu, maombolezo, na kusaga meno. Ili kuenenda katika njia ya Yesu Kristo, lazima tuachane na njia ya kimwili. Yesu alisema, “Mtu yeyote akitaka kuwa mfuasi wangu, lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.” (Mathayo 16:24). Je, kujikana nafsi kunamaanisha nini?

Baadaye, Africa 4 minutes

Injili ya Yohana 10:1-18 Je, umewahi kumsikia mtu akiita jina lako lakini hukufahamu sauti yake ilikuwa ikitokea wapi? Au, hukuweza kusikia sauti kwa maana kulikuwa na kilele nyingi pande zote? SIKILIZA………sauti inakuita. Wewe! Wewe ni nani? Jina lako ni nani? Ulitoka wapi? Unakwenda wapi? Unajua jina la kijiji chako. Inawezekana hujawahi kwenda mahali pengine po pote. Lakini wewe wafahamu kwamba kijiji chako ni sehumu ya nchi kubwa, na nchi zote ni sehemu za ulimwengu mkubwa.

Wokovu 6 minutes

Tunaishi katika ulimwengu ambamo kila mmoja hupenda kutoa udhuru. Karibu kwa kila jambo linalogusa moyo wako hutaki kukubali au kuukabili ukweli jinsi ulivyo, kwa hiyo unatafuta njia ya kujitetea, ukidhania kwamba utetezi wako utakuweka huru. Je, unafikiri udhuru zako zitakuweka huru mbele za Mungu? Je, kuokolewa kunao udhuru? Visingizio ulivyo navyo kwa uhakika havitakuweka huru. Adamu na Hawa walipotenda dhambi, kila mmoja alijaribu kumtupia mwenzake lawama ya dhambi iliyotendeka, wakidhania kwamba Mungu angeachilia dhambi yao kwani wametoa sababu ni kwa nini waliingia dhambini. Lakini bado twasoma katika Biblia kwamba Mungu aliendelea kuwaadhibu tu. Mungu hazikubali udhuru zetu, hata zipangiwe kwa hila ya namna gani, au hata ukijifanya uonekane kuwa msafi kiasi gani. (Mwanzo 3:9-19; Wagalatia 6:7-8).

Maisha Ya Kikristo 6 minutes

Kila mahali watu wote hutamani kuwa na vitu vya kupendeza kwa maisha yao. Kila mmoja angependa kuwa na chakula kizuri, na cha kutosha kugawanya kwa marafiki na wageni; nguo zilizokamilika, na za kutosha kubadili kwa wakati mbalimbali; nyumba nzuri, imara na kubwa ya kutosha, yenye paa nzuri kwa majira yote. Pia tunatarajia kuwa na kiasi cha fedha mkononi ili kukabili matumizi yote, shughuli zetu, kwa dawa ukijitokeza ugonjwa, na hata ya kutosha kusafiria kuwaona marafiki mahali pengine. Kila mmoja hutaka dhamana ya kufanikiwa, hata kuwa na pesa za ziada mkononi kumaliza shida za dhorura.

Maisha Ya Kikristo, Africa 10 minutes

Bwana Yesu alikuja ulimwenguni kuwaokoa wanadamu kutoka kwa dhambi zao. “Bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa akawa ana mfano wa wanadamu” (Wafilipi 2:7). Alikufa kwa ajili ya dhambi za watu wote ulimwenguni, alizikwa na akafufuka tena (1Wakorintho 15:4), kisha akapaa kwenda mbinguni tena (Matendo 1:9). Mitume walimwona na pia waumini zaidi ya mia tano, baada ya kufufuka. Baada ya kupaa kwenda mbinguni, malaika wawili waliwaambia mitume kwamba kurudi kwake kutafanana na kupaa kwake. Ni Mungu tu ndiye anayefahamu ni lini Bwana atarudi. Huenda itakuwa ni jioni au usiku wa manane, au wakati wa asubuhi au alasiri. (Marko 13:35) “Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja” (Mathayo 24:44).

Mbeleni 3 minutes

Kabla ya muda haujakuwepo Mungu alikuwepo. Aliumba dunia na kila kitu kilichomo. Katika upendo wake, Mungu akaumba mwanadamu kwa sura yake mwenyewe akawaweka kwenye bustani nzuri. Wanadamu hawakutii maelekezo ya Mungu. Kutokutii huku kulikuwa ni dhambi iliyowatenganisha mbali na Mungu. Aliwaambia kwamba wanapaswa kutoa dhabihu za wanyama wadogo wasio na madoa yoyote kwa ajili ya dhambi zao. Dhabihu hizi hazikulipia dhambi zao bali zilielekeza dhabihu ya mwisho ambayo Mungu angetoa. Siku moja Mungu angetuma mwanawe Yesu duniani awe dhabihu ya mwisho.

Yesu, Color 3 minutes