Vipeperushi

Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na nchi. Aliumba jua, mwezi, na nyota, na pia mimea na wanyama. Siku ya sita, aliumba mtu kwa mfano wake na akampulizia puani pumzi ya uhai. Mtu huyu wa kwanza alikuwa Adamu, na jina la mkewe aliitwa Eva. Mungu aliwapa makao ya kuishi katika bustani nzuri ya Edeni. Mungu aliwapenda Adamu na Eva, nao walimpenda Mungu. Mungu alimwagiza Adamu kuitunza bustani. Mungu aliwaambia kua wanaweza kula chochote watakacho isipokuwa kwa mti wa ujuzi wa mema na mabaya, na ya kuwa watakufa kama hawatatii.

Baadaye, Injili, Mbinguni, Color 3 minutes

Imeandikwa na John Reynolds Mojawapo ya mifano iliyohai na ya kuvutia kabisa ya kurudishiwa uhai wa mtu aliyekwisha kufa ambao nimewahi kuufahamu ulikuwa ni ule wa George Lennox, mwizi stadi wa farasi kutoka Jimbo la Jefferson (Marekani). Alikuwa akitumikia kifungo chake cha pili. Jimbo la Sedwick lilimpeleka gerezani kwa mara ya kwanza kwa kosa hilo hilo – wizi wa farasi.

Baadaye 11 minutes
Wokovu 13 minutes

Je, wewe ni mwenye furaha? Au hofu na hatia huondoa furaha yako yote? Je, ungetamani kuondoa hatia yako, lakini hujui kwa njia gani? Huenda unajiuliza, “Je, nitawahi kuwa mwenye furaha tena?” Ninayo habari njema kwa ajili yako. Kuna Mmoja awezaye kukusaidia, kusamehe dhambi zako, na kukupa furaha ya daima. Jina lake ni Yesu. Ngoja nikuambie habari zake. Mungu ndiye mwenyewe aliyeumba ulimwengu na vitu vyote vilivyomo. Alikuumba wewe na mimi.

Yesu 3 minutes

Lengo la Biblia Takatifu silo kuangalia hasa Shetani na kazi zake. Japokuwa tunapata mengi kwenye Biblia yanayofunua tabia zake na kazi zake. Wakati fulani Shetani alikuwa malaika, lakini aligeuka kinyume cha Mungu, Muumba wake, na akatamani kuwa kama Mungu. Matendo ya ufalme wa giza wa Shetani siyo mageni. Yanaonyesha dhahiri jitihada za Shetani kwa miaka kupingana na Ufalme wa Mungu. Anatoa mbadala wa kile ambacho Mungu anatimiliza kwa kupitia nguvu za Roho Mtakatifu.

Wokovu 6 minutes

Injili ya Yohana 10:1-18 Je, umewahi kumsikia mtu akiita jina lako lakini hukufahamu sauti yake ilikuwa ikitokea wapi? Au, hukuweza kusikia sauti kwa maana kulikuwa na kilele nyingi pande zote? SIKILIZA………sauti inakuita. Wewe! Wewe ni nani? Jina lako ni nani? Ulitoka wapi? Unakwenda wapi? Unajua jina la kijiji chako. Inawezekana hujawahi kwenda mahali pengine po pote. Lakini wewe wafahamu kwamba kijiji chako ni sehumu ya nchi kubwa, na nchi zote ni sehemu za ulimwengu mkubwa.

Wokovu 6 minutes

Tunaishi katika ulimwengu ambamo kila mmoja hupenda kutoa udhuru. Karibu kwa kila jambo linalogusa moyo wako hutaki kukubali au kuukabili ukweli jinsi ulivyo, kwa hiyo unatafuta njia ya kujitetea, ukidhania kwamba utetezi wako utakuweka huru. Je, unafikiri udhuru zako zitakuweka huru mbele za Mungu? Je, kuokolewa kunao udhuru? Visingizio ulivyo navyo kwa uhakika havitakuweka huru. Adamu na Hawa walipotenda dhambi, kila mmoja alijaribu kumtupia mwenzake lawama ya dhambi iliyotendeka, wakidhania kwamba Mungu angeachilia dhambi yao kwani wametoa sababu ni kwa nini waliingia dhambini. Lakini bado twasoma katika Biblia kwamba Mungu aliendelea kuwaadhibu tu. Mungu hazikubali udhuru zetu, hata zipangiwe kwa hila ya namna gani, au hata ukijifanya uonekane kuwa msafi kiasi gani. (Mwanzo 3:9-19; Wagalatia 6:7-8).

Maisha Ya Kikristo 6 minutes

Bwana Yesu alikuja ulimwenguni kuwaokoa wanadamu kutoka kwa dhambi zao. “Bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa akawa ana mfano wa wanadamu” (Wafilipi 2:7). Alikufa kwa ajili ya dhambi za watu wote ulimwenguni, alizikwa na akafufuka tena (1Wakorintho 15:4), kisha akapaa kwenda mbinguni tena (Matendo 1:9). Mitume walimwona na pia waumini zaidi ya mia tano, baada ya kufufuka. Baada ya kupaa kwenda mbinguni, malaika wawili waliwaambia mitume kwamba kurudi kwake kutafanana na kupaa kwake. Ni Mungu tu ndiye anayefahamu ni lini Bwana atarudi. Huenda itakuwa ni jioni au usiku wa manane, au wakati wa asubuhi au alasiri. (Marko 13:35) “Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja” (Mathayo 24:44).

Mbeleni 3 minutes

Kabla ya muda haujakuwepo Mungu alikuwepo. Aliumba dunia na kila kitu kilichomo. Katika upendo wake, Mungu akaumba mwanadamu kwa sura yake mwenyewe akawaweka kwenye bustani nzuri. Wanadamu hawakutii maelekezo ya Mungu. Kutokutii huku kulikuwa ni dhambi iliyowatenganisha mbali na Mungu. Aliwaambia kwamba wanapaswa kutoa dhabihu za wanyama wadogo wasio na madoa yoyote kwa ajili ya dhambi zao. Dhabihu hizi hazikulipia dhambi zao bali zilielekeza dhabihu ya mwisho ambayo Mungu angetoa. Siku moja Mungu angetuma mwanawe Yesu duniani awe dhabihu ya mwisho.

Yesu, Color 3 minutes