Vipeperushi
Amani, amani iko wapi—kwa mataifa, nyumbani kwetu, na zaidi ya yote kwa mioyo yetu? Kilio hiki kikuu kimesikika kwa vizazi. Je, ni kilio cha moyo wako pia? Watu wamechoka na kuhangaika. Bila shaka kuna haja ya mwongozo na ushauri, usalama na kujiamini. Tunahitaji na kutaka akili yenye utulivu. Akili yenye utulivu—Ni hazina iliyoje! Je, hazina hii inaweza kupatikana katika ulimwengu wenye mizozo na kukata tamaa, wenye misukosuko na matata?
Mwanamume mmoja kijana alifiwa mke wake wakati mtoto wake wa kiume akiwa bado mdogo. Kwa maangalizi ya makini na ya woga kabisa huyo baba aliweza kumlea yule mtoto. Kwa kuwa kijana alikuwa ni mboni ya jicho lake, alimpa vitu vingi, na alimpa chakula bora kabisa kilichokuwa kinapatikana. Baada tu ya yule mwanaume kupona na mawazo ya kumpoteza mke wake mpendwa, mtoto wake wa kiume aliugua na alikuwa na hali mbaya sana. Daktari aliagiza dawa ya kuponya ugonjwa wake. Dawa ile ilikuwa na ladha ya uchungu, kwa hiyo yule kijana hakutaka kuinywa. Kila mara baba yake alikuwa anamlazimisha kunywa ile dawa.
Yesu anasema kwamba milango ya mbinguni imefungwa dhidi yako isipokuwa unazaliwa mara ya pili. Kwa hiyo twauliza: “Rafiki, umezaliwa mara ya pili?” “Muumini wa kanisa, umezaliwa mara ya pili?” Ikiwa hapana, basi umepotea. Kwa maana Yesu anasema, “Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu” (Yohana 3:3). Kwa kweli hakuna mtu anayetaka kufa akiwa mwenye dhambi, au kupotea; basi hamna budi kuzaliwa mara ya pili.
Mungu wa Kweli Ndiye Muumbaji
Tunasoma katika Biblia, “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Na Mungu akawabarikia” (Mwanzo 1:27-28). Mungu alimwumba mwanadamu, uumbaji wake wa hali ya juu kabisa na wa hekima, “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai” (Mwanzo 2:7). Anastahili wanadamu wamtumikie na kumsifu Yeye. “Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa” (Ufunuo 4:11). Kwa hiyo, viumbe vyake vingemwabudu Yeye, na Yeye tu, “…kumwabudu katika roho na kweli” (Yohana 4:24).
Tukabili hali halisi. Maovu ya kutisha - pombe, madawa ya kulevya, na zinaa - vinatishia na kuharibu kile kilichoubwa na Mungu kuwa kizuri. Vinakamata na kuwavuta wadogo kwa wakubwa kama mikono ya pweza mkubwa inavyoshika. Maambukizo kwa jamii ya leo ni makadirio makubwa. Watu wengi wamelegea bila nanga na kuachwa na laana ya pombe, madawa ya kulevya, na zinaa, wakielekea maangamizi ya milele. Watu wanavutwa upesi na wenzao, pamoja na matangazo yanayotolewa na video, radio, na magazeti kuhusu maovu hayo. Akili inashambuliwa mpaka inachanganyakiwa na kukaa na mawazo ya machafuko ambayo matokeo yake ni uharibifu wa kiroho na kimwili.
Hili ni swali zuri sana ambalo kila mmoja anapaswa kujiuliza. Biblia inaongelea njia kuu mbili tu; njia ya kwenda Mbinguni na njia ya kwenda Jehanamu. Mbinguni ni sehemu yenye kila kitu kizuri, na ni makao ya Mungu. Jehanamu ni mahali pa dhambi na maharibifu yasiyo na mwisho. Ni sehemu iliyoandaliwa kwa ajili ya Shetani na watoto wake. Je,nifanye nini ili niweze kufika mahali ambapo ni nyumbani mwa Mungu? Kama wewe si mkristo sahihi, na haujazaliwa kwa mara ya pili, basi unahitaji wokovu.
Hili ni swali zuri sana ambalo kila mmoja anapaswa kujiuliza. Biblia inaongelea njia kuu mbili tu; njia ya kwenda Mbinguni na njia ya kwenda Jehanamu. Mbinguni ni sehemu yenye kila kitu kizuri, na ni makao ya Mungu. Jehanamu ni mahali pa dhambi na maharibifu yasiyo na mwisho. Ni sehemu iliyoandaliwa kwa ajili ya Shetani na watoto wake. Je,nifanye nini ili niweze kufika mahali ambapo ni nyumbani mwa Mungu? Kama wewe si mkristo sahihi, na haujazaliwa kwa mara ya pili, basi unahitaji wokovu.
“Tazama wapendezwa na kweli iliyo moyoni” (Zaburi 51:6). Uaminifu ni adili la ukweli linalofungamana na mambo yote ya maisha. Kwa hakika uaminifu ni jambo la moyoni, pia ni fundisho la msingi la Injili ya Yesu Kristo. Mungu anajua mawazo na makusudi ya moyo. Anatambua ukweli kama msingi muhimu kwa maana yeye ni Mungu wa ukweli. (Kumb. 32:4) Hakika atabariki uaminifu uliokamilika wa mioyo yetu. Je, unayo tabia ya kusema ukweli wakati mambo yako yangedhihirika, lakini ukawa si mwaminifu wakati ambao hakuna atakayekugundua? Je, kwa makusudi ungeweza kumridhisha mtu kwa ushawishi usio wa kweli?
Je, wajua kwamba kuna mtu ambaye hujua yote juu yako? Ni Mungu aliyeumba ulimwengu na vitu vyote vilivyomo. Yesu, Mwana wa Mungu, pia hujua yote ambayo umeshafanya. Yeye hujua yaliyopita, ya leo, na yajayo. Yeye anakupenda na alikuja ulimwenguni kukuokoa kutoka dhambini. Anao mpango wa uzima wako ili kukuletea furaha. Siku moja Yesu alikuwa akitembea na rafiki zake alifikia kijiji cha Samaria. Yesu alikaa kando ya kisima wakati rafiki zake walienda kununua chakula. Yesu alipokuwa amekaa pale, mwanamke mmoja alikuja kuteka maji kisimani. Yesu alimwambia, “Naomba unipe maji ninywe.”
Je, wajua kwamba kuna kitabu ambacho hueleza jinsi dunia ilivyoanzishwa? Maneno ya kwanza ya kitabu hiki ndiyo, “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi”. Kufuata maneno haya inaeleza jinsi dunia ilivyoumbwa na kuhusu mwanamume wa kwanza na mwanamke walioishi duniani. Inatuambia si tu kuhusu mwanzo wa muda, lakini pia ni kile kitakachotokea maisha haya yakiisha. Katika kitabu hiki chote, twasoma jinsi tunavyopaswa kuishi ili tuandaliwe kwa maisha baada ya kifo.